Thursday, April 16, 2015

SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA KILELE CHA SIKU YA ELIMU NA MAZINGIRA KWA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI MANISPAA YA ILALA

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Maktaba wakicheza ngoma wakati wa sherehe za Maazimisho ya Kilele cha Siku ya Elimu Wilaya ya Ilala na Kilele cha Maadhimisho ya Mazingira kwa Shule za Msingi na Sekondari za Manispaa ya Ilala 'Mazingira Bora Kwa Elimu  Bora'.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Diamond,  Hashimu Semvua, akikabidhiwa Tuzo ya kwanza ya Mazingira ya Kata ya Gerezani  Manispaa ya Ilala, na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi.
 Mkuu wa Wilaya Ilala, Raymond Mushi, akifunga rasmi Siku ya Elimu na Kilele cha Maazimisho ya Mazingira Shule za  Msingi na Sekondari Manispaa ya Ilala.
 Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi,  akisikiliza maelezo kutoka kwa mwanafunzi Fatuma Omari mwanafunzi wa kidatu cha pili  shule ya Sekondari  Benjameni Mkapa, wakati alipokuwa akitembelea maonyesho ya Sayansi ya wanafunzi hao katika sherehe hizo za kilele cha Siku ya Elimu Wilaya ya Ilala. Aliyeshika Maiki ni Mwalimu Elizabeth Mapela wa elimu maalum.
Mkurungezi wa Manispaa ya Ilala Isaya Mwangurume, akimkaribisha mgeni rasmi (kushoto kwake) Kulia ni Mwenyekiti wa Uchumi na Hunduma za Jamii Manispaa ya Ilala, Angel Malembeka. 
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Diamond,  Hashimu Semvua, akipongezwa na walimu wenzake baada ya kupokea Tuzo ya kwanza ya Mazingira ya Kata ya Gerezani  Manispaa ya Ilala. Picha na Miraii Msala

No comments:

Post a Comment