Tuesday, September 9, 2014

*RAIS KIKWETE AHITIMISHA MAZUNGUMZO YAKE NA UJUMBE WA KITUO CHA DEMOKRASIA IKULU NDOGO DODOMA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo na ujumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) baada ya kumalizika kwa  awamu ya pili ya mazungumzo nao Ikulu Ndogo mjini Dodoma jana.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) baada ya kumalizika kwa  awamu ya pili ya mazungumzo nao Ikulu Ndogo mjini Dodoma jana.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) baada ya kumalizika kwa  awamu ya pili ya mazungumzo nao Ikulu Ndogo mjini Dodoma jana.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na  Wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) baada ya kumalizika kwa  awamu ya pili ya mazungumzo nao Ikulu Ndogo mjini Dodoma jana. Picha na IKULU

WATANO WAFIKISHWA KIZIMBANI KWA WIZI WA GARI LA IKULU KENYA

WATU watano akiwemo raia mmoja wa Uganda pamoja na fundi mmoja wa magari wameshitakiwa kwa kosa la wizi wa gari la msafara wa ulinzi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta nchini Kenya. 
Watu hao pia walishitakiwa kwa kumuibia gari inspekta wa polisi David Machui, aliyekuwa akiendesha gari hilo aina ya BMW 735 mnamo Agosti 26 mjini Nairobi lilipoibwa. 
Washukiwa hao wote walikanusha madai hayo kwamba walihusika katika wizi wa gari hilo. Kila mshukiwa aliachiliwa kwa kima cha shilingi milioni 5 isipokuwa mwanamume mmoja aliyesemekana kuwa na kesi tofauti mahakamani. 
Raia wa Uganda Robert Mande Ochan, aliamrishwa na mahakama kutoa dhamana ya shilingi milioni mbili ili aweze kuachiliwa. Gari hilo lilipatikana mjini Kampala Uganda na kurejeshwa nchini Kenya siku ya Ijumaa. 
Washukiwa hao walioiba gari hilo wakiwa wamejihami, wanashukiwa kuwa sehemu ya mtandao wa wezi wa magari wakiendeshea kazi yao nchini Kenya, Burundi, DRC , Tanzania na Uganda. 
Kikundi hicho kiko na wahalifu, maafisa wafisadi wa kutoza ushuru na mafundi wa magari. Polisiwa wa Uganda walipata hari hilo baada ya mpenzi wa mshukiwa mmoja kumuwekea mtego ambao ulimfikisha kwa polisi, katika mtaa wa Wandegeya, mjini Kampala. 
Maswali yamekuwa yakiulizwa kuhusu afisaa wa polisi aliyeruhusiwa kuendesha gari la serikali kama gari lake binafsi, wakati utaratibu unasema kuwa magari yote ya serikali yanapaswa kuegeshwa katika kituo cha polisi kilicho karibu na dereva wa gari hilo.