Thursday, April 16, 2015

MASHABIKI WA SIMBA KUISHANGILIA YANGA

Katika kile kinachotarajiwa na mashabiki wengi wa soka la Bongo ni tukio la mashabiki wa timu Kongwe za nchini Yanga na Simba, siku watakapoingia uwanjani kwa lengo la kuishangilia timu pinzani wakatiikicheza.

Kutokana na Ligi Kuu ya Tanzania bara kuwa ngumu msimu huu, huku timu za Yanga na Mabingwa watetezi Azam Fc wakifukuzana katika mbio hizo za kuwania ubingwa na kutofautiana kwa Pointi saba na Simba nao wakikesha huku wakiiombea mabaya Azam na wakijitahidi angalau kumaliza Ligi wakiwa nafasi ya pili, hii ndiyo hasa sababu kubwa itakayowabadilisha mashabiki wa timu hizi kushangilia wapinzani wa jadi.

Yanga inaongoza Ligi hiyo ikiwa na jumla ya Pointi 46, baada ya kucheza mechi 21, wakifuatiwa na Azam Fc wenye Pointi 39,nao pia wakicheza mechi 21 huku Simba wakiwapumulia Azam Fc wakiwa na Pointi 35 nao pia wakicheza mechi 21 na Kagera Sugar wakifuatia wakiwa na Pointi 31 wakicheza mechi 22.

Kwa matokeo hayo Mabinwa watetezi Azam Fc bado wana mechi ngumu mkononi ambazo ni kati yao na Yanga na Simba, ambapo mechi hizi hsa ndizo zitawasilimisha mashabiki wa timu za jadi watakaolazimika kushangilia timu pinzani.

Siku ya mechi ya Yanga na Azam Fc, mashabiki wa Simba watalazimika kuishangilia Yanga ili Yanga ishinde na Azam Fc wapoteze mchezo ili Simba iendelee kuwa na uhakika wa kuipata nafasi ya pili ili iweze kushiriki michuano ya Kimataifa.

Na siku ya mechi ya Simba na Azam Fc, mashabiki wa Yanga nao watalazimika kuishangilia Simba, ili Azam Fc waendelee kuchechemea katika mbio hizo za kuwania ubingwa

No comments:

Post a Comment