Thursday, April 16, 2015

MIMI SIJAFA NI UZUSHI WA WAJINGA WA MITANDAO TU: HUSSEIN MACHOZI

Habari zilizoenea katika mitandao ya kijamii kuhusu Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Hussein Machozi, zikimzushia kifo si za kweli na ni jambo ambalo linatakiwa kukemewa kwa nguvu zote kwani ni upotoshaji wa habari.

Akizungumza na mtandao huu kwa njia ya Simu muda mchache uliopita Machozi alisema kuwa amesikitishwa na uzushi huo ulioenezwa kwenye mitandao ya Kijamii, na kuwaondoa hofu Ndugu, Jamaa, Marafiki na Mashabiki wake kuwa yupo fiti.

''Mimi nipo fiti na naendelea na majukumu yangu ya kila siku kama kawaida, hizo ni habari za uzushi tu ambazo sielewi lengo lake ni nini, labda ndo kunitakiwa maisha marefu lakini si jambo zuri na hata huyo alieanzisha na kusambaza kwenye mitandao alikuwa na lengo lake ambalo mimi na hata wewe mwandishi hatulijui, 

Hivyo kwa kuwa ameshakamilisha dhamira yake na wengi wameshitushwa na habari hii, basi nadhani ameshatimiza alilokuwa amekusudia, hivyo tumuachia Mwenyezi Mungu tu''. alisema Machozi

Habari za uzushi kama hizi zimekuwa zikienea kwa kasi katika mitandao ya Kijamii, ambapo siku za hivi karibuni pia ilisambazwa habari katika mitandao kuwa aliyekuwa Kocha wa Simba, Mzee Kibaden amefariki, jambo ambalo halikuwa la kweli, hivyo wanajamii tuungane na hasa watumiaji wa mitandao kukemea watu hawa wasiouwa maana halisi  na matumizi ya mitandao ya kijamii.

TUKIUNGANA TUNAWEZA KUWAKOMESHA

No comments:

Post a Comment