Friday, April 17, 2015

BAADA YA AJALI YA JANA MTO WAMI, LEO NI HUKO KIWILA MKOANI MBEYA, HICE YAUA WATU KADHAA

Habari zilizotufikia Mtandao huu hivi punde zinasema kuwa ajali nyingine mbaya imetokea huko Kiwila maeneo ya Uwanja wa Ndege Wilaya ya Rungwe, Mkoani Mbeya, baada ya Hice iliyokuwa imebeba abiria kutumbukia mtoni na kudaiwa kuuwa watu ambao idadi yake amili kbado haijapatikana.

Aidha imeelezwa kuwa katika ajali hiyo mpaka sasa ni watu wawili akiwemo Kondakta wa Hice hiyo waliookolewa huku ikielezwa kuwa hadi sasa tayari jumla ya miili 22, imeshaopolewa kutoka kwenye Mto huo. 

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijaweza kufahamika, lakini pia ikielezwa kuwa Hice za jijini Mbeya leo zilianza kutoa huduma ya usafiri baada ya Daladala nyingi aina ya Coaster kugoma kutoa huduma hiyo leo.
Hice hiyo inavyoonekana ikiwa mtoni baada ya kuanguka huku raia wakiishangaa.
Eneo la ajali hiyo katika daraja hili ambapo iliacha njia na kutumbukia 
Wananchi waliofika kutoa msaada wakiopoa miili na kuihifadhi eneo hili.
Mpaka sasa Miili iliyokwishaopolewa ni 22.
Gari la Polisi likiwa eneo la tukio kubeba miili. Picha kwa Hisani ya Mdau aliyeko Mbeya

VIJANA WA CCM IRINGA WAMPA NGUVU KATIBU WA MKOA HASSAN MTENGA KUKOMBOA JIMBO, LA IRINGA MJINI

Mtenga katika kikao na baadhi ya vijana hao



KIU ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa kukomboa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu inazidi kuongezeka, baada ya umoja wake wa vijana (UVCCM Manispaa ya Iringa) kuahidi kuongeza nguvu ili kuufanikisha mkakati huo.
CCM ililipoteza jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa Mchungaji Msigwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayekaribia kumaliza muda wake.
Katika kikao kilichozikutanisha sekretarieti za umoja huo kutoka katika kata zote 18 za manispaa ya Iringa, Mwenyekiti wa UVCCM wa manispaa hiyo, Kaunda Mwaipyana alisema; “katika kukisaidia chama kushinda uchaguzi huo, kauli mbiu yetu ni chama kwanza mtu baadaye.”
“Tutapita katika matawi na kata zetu zote, tutafanya vikao, mikutano ya hadhara na kuwakumbusha vijana wajibu wa kukipigania chama chao ili mkakati wa kulikomboa jimbo ufanikiwe,” alisema.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga aliwaongezea hamasa vijana hao kwa kuwapa seti 60 za jezi na mipira watakazozitumia kuwahamasisha vijana hao kupitia mchezo wa soka.
“CCM ina vijana wengi sana katika jimbo hili, mnahitaji kukutana na kujipanga, tumieni mbinu zote za kukutana, iwe  vikao, mikutano na hata michezo na ndio maana nimewapa msaada huu,” alisema.
Aliwataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwenye vikao visivyo rasmi vya maeneo yao wanayoishi na kuitetea CCM kwasababu majibu ya hoja nyingi za wapinzani wanayo.
Akiwakabidhi jezi hizo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Mkoa wa Iringa, Ephraim Mhekwa alisema  CCM inayo nafasi ya kulikomboa jimbo hilo kama itajipanga vizuri.
“Pamoja na kwamba wapinzani walipata viti 65 katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka jana, wasisahau kwamba CCM ilipata viti 126; hesabu hiyo inadhihirisha chama chetu kinaungwa mkono mara mbili yao,” alisema.
Aliwataka vijana hao kuweka bendera za chama hicho kila panapostahili katika mitaa yote na akawasihi wasikubali kutumika na kukigawa chama kwa maslai ya wachache.
Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mahamudu Madenge alisema CCM itaendelea kuwepo hata kama watu wasiotaka kufuata utaratibu wataondoka.
“Wameondoka wengi, wengine hii leo ni viongozi wa vyama vikubwa vya siasa. Pamoja na kuondoka kwao CCM ipo pale pale na inaendelea kupata wanachama,” alisema