Wednesday, April 29, 2015

WIKI YA ELIMU, NA UZINDUZI WA TUZO YA TAALUMA YA MKUU WA MKOA IRINGA

Kauli Mbiu: NJOMBE Na 1 INAWEZEKANA.
‘’Elimu Bora ni Haki ya kila Mtoto kwa Maendeleo ya Taifa. Njombe Kuwa Na.  1. Inawezekana.’’ Hiyo ilikuwa ni Kauli Mbiu iliyopamba Kilele cha maadhimisho ya wiki ya Elimu Kimkoa katika Mkoa wa Njombe siku ya tarehe 27/04/2015; Maadhimisho hayo yaliambatana na Uzinduzi wa Tuzo ya Taaluma ya Mkuu wa Mkoa, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi alikuwa Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Turbo ndani ya Halmashauri ya Mji Njombe.
‘’Tuzo hiyo ina  dhamira ya kuufanya Mkoa wa Njombe kuongoza Kitaaluma kwani haki tunayo,uwezo tunao na wajibu tunao’’ Alisema Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi.
Tuzo hizo ziliambatana na ugawaji wa zawadi mbalimbali kwa Shule zenye ufaulu wa juu,Shule zilizoongeza ufaulu,Wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani ya Sekondari na Waalimu wenye ufaulu wa juu kwenye masomo wanayofundisha.
Dkt Nchimbi pia amewakaribisha wadau mbalimbali wa Elimu,Makampuni na Taasisi Mbalimbali  kujitokeza katika kuzienzi na kutoa Tuzo hizo huku zikibeba majina ya Taasisi zao.
Maadhimisho hayo pia yalipambwa na shughuli mbalimbali ikiwemo kutembelea mabanda ya shule  nakuona shughuli zinazofanywa na wanafunzi na ugawaji wa zawadi kwa waendesha pikipiki bora kwa Mkoa wa Njombe.

Imetolewa na Afisa Habari
H/Mji Njombe.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment