Friday, April 17, 2015

BAADA YA AJALI YA JANA MTO WAMI, LEO NI HUKO KIWILA MKOANI MBEYA, HICE YAUA WATU KADHAA

Habari zilizotufikia Mtandao huu hivi punde zinasema kuwa ajali nyingine mbaya imetokea huko Kiwila maeneo ya Uwanja wa Ndege Wilaya ya Rungwe, Mkoani Mbeya, baada ya Hice iliyokuwa imebeba abiria kutumbukia mtoni na kudaiwa kuuwa watu ambao idadi yake amili kbado haijapatikana.

Aidha imeelezwa kuwa katika ajali hiyo mpaka sasa ni watu wawili akiwemo Kondakta wa Hice hiyo waliookolewa huku ikielezwa kuwa hadi sasa tayari jumla ya miili 22, imeshaopolewa kutoka kwenye Mto huo. 

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijaweza kufahamika, lakini pia ikielezwa kuwa Hice za jijini Mbeya leo zilianza kutoa huduma ya usafiri baada ya Daladala nyingi aina ya Coaster kugoma kutoa huduma hiyo leo.
Hice hiyo inavyoonekana ikiwa mtoni baada ya kuanguka huku raia wakiishangaa.
Eneo la ajali hiyo katika daraja hili ambapo iliacha njia na kutumbukia 
Wananchi waliofika kutoa msaada wakiopoa miili na kuihifadhi eneo hili.
Mpaka sasa Miili iliyokwishaopolewa ni 22.
Gari la Polisi likiwa eneo la tukio kubeba miili. Picha kwa Hisani ya Mdau aliyeko Mbeya

No comments:

Post a Comment